user_mobilelogo

Party Emblem

Party Flag

 

Youth League

Contact us


Communist Party Marxist - Kenya (CPM-K)
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
P.O Box 101011-00101 Nairobi, Kenya.
 

Let's Get Social

          

 

Related Social Links

 Revolutionary Youth League (RYL)
   
 Revolutionary Student Commission
    
 Revolutionary Women League
 Pio Gama Pinto Institute 

Support CPM-K 

membership

Publications

 

 

 

 Grab a Copy

 

CPM-K Memberships

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Mau Mau

Mau Mau, jeshi la Uhuru na Mashamba

Kilele cha mapambano dhidi ya ukoloni-mkongwe

Jazanda ya wazalendo na uzalendo

Mau Mau, mashujaa halisi wa nchi yetu

Wakakataa kutembea katika njia ya kina Jomo Kenyatta

Njia ya wasabili ya kuomba uhuru wa kuomba

Njia ya kutegemea adili ya wagandamizaji

Njia ya kuongozwa na masilahi ya ulafi na uroho

Njia ya kukana mapambano ya silaha katika hali ya ufashisti

Mau Mau wakulima na wafanyikazi wa Kenya

Wanaume kwa wanawake wazee kwa vijana

Walichagua barabara ya kimapinduzi ya uhuru

Mau Mau waliokula kiapo cha ukombozi

Kiapo cha kuwaunganisha na kuwashikanisha kwa mapambano

Mapambano ya kupigania mashamba na uhuru wetu

Mapambano ya kupigania heshima na utu wa mtu mweusi

Mapambano ya demokrasi na haki za binadamu

Mapambano ya kuung'oa ukoloni nchini kwetu

Maelfu kwa maelfu ya wazalendo wa Kenya

Waliowacha kila kitu na kuitikia mwito

Mwito wa kujitoma milima Kenya na Nyandarua

Mwito wa kusambaa katika miji na vijiji vya nchi yetu

Kuendeleza vita vya kigorila dhidi ya wakoloni na vibaraka vyao

Waliovumilia njaa na kiu na baridi na upweke na dhiki tilatila

Wakajasiri kuwindwa na kukamatwa na kuhamishwa

Waliokuwa tayari kuvumilia kukamatwa na kufungwa

Mau Mau, maelfu kwa maelfu waliwawa na wakoloni

Mau Mau, ni wangapi mashujaa wetu waliyonyongwa!

Mau Mau, kiboko cha makaburu na mahomugadi

Mau Mau, kwa damu yenu, kwa kujitolea mhanga kwenu

Enyi wananchi wakereketwa wa taifa letu

Kwa msimamo wenu

Kwa mwelekeo wenu

Kwa harakati zenu

Kwa vita sahihi mlivyopigana

Tuko pahali tulipo sasa, hatua kubwa mbele

Ukoloni-mkongwe haupo tena nasi, mliukwamua Mau Mau

Kwenu Afrika ikapata mfano mzuri wa kuiga

Mfano wa kupigania ukombozi kwa kutumia silaha

Mau Mau, Jeshi la uhuru na Mashamba

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu ya kila aina

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Mau Mau

Vilikuwa vita vya kupigania uhuru wa kitaifa

Vita vya wananchi na wananchi kwa ajili ya wananchi

Navyo vita vya wananchi vilizaa mashujaa wengi, wengi sana

Mashujaa waliochipuka katika msitari wa mbele

Mashujaa walioteuliwa na ari na shauku ya kujitolea mhanga

Kujitolea mhanga kutumikia vita vya ukombozi

Mashujaa waliodhihirisha ujemedari na uhodari

Wa kuongoza jeshi lililokuwa la wananchi wa Kenya

Mashujaa waliokuwa mashuhuri katika uwanja wa vita

Kwa usanii wa kuzalisha hila na mbinu za kuwachapa maadui

Mashujaa wa siasa na itikadi ya wanaonyanyaswa

Waliohamasisha umma kwa maneneo na vitendo vyao

Mashujaa wa kutetea haki na ukweli na maslahi ya wengi

Waliochagua kuishi maisha ya utu ya kupinga dhuluma

Mashujaa kwa mapenzi ya nchi yetu na ukombozi wake

Kwa maendeleo ya Kenya na furaha  ya kila raia

Kwa imani na amani ya wanaonyonywa na kunyanyaswa

Mashujaa waliokuwa wakipiga konde nyoyo kila wakati

Waliopambana dhidi ya kulegalega na kukata tamaa

Mashujaa ambao baada ya kukamatwa na wakoloni

Wakiwa mikononi mwa makaburu na mahomugadi

Wakiteswa katika magereza ya wadhalimu wa nchi yetu

Katikati ya ufashisti wa dola la Waingereza

Walivumilia yote kwa ujasiri usiyo na kifani

Walikataa kusaliti kiapo cha kupigania uhuru

Wakadinda kukana vita vya haki vya ukombozi wa Kenya

Wasikubali kutoboa siri wala kusaliti makomredi wao

Na hata waliponyongwa na kuuawa kinyama kabisa

Mashujaa wetu walikufa kwa fahari

Wakawawachia wakoloni na vibaraka wao aibu ya milele

Ni wengi mashujaa wa Mau Mau, wengi sana

Kwani Mau Mau ni wanati, wananchi wazalendo wakereketwa

Mau Mau, ushujaa wa mamilioni

Ya wakulima na wafanyikazi

Wanaume kwa wanawake wazee kwa vijana

Ambao kwa moyo wa harambee uzalendo na kujitegemea

Walifunga sura  ya ukoloni-mkongwe katika nchi yetu

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu ya kila aina

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Kimaathi

Dedan Kimaathi

Dedan Kimaathi wa Waciuri

Mkuu wa jeshi la Uhuru na Mashamba

Kati ya majemedari wa Mau Mau Kimaathi ali ni gogo

Baina ya mashujaa wa uhuru hakika Dedan Kimaathi ni nyota

Nyota iliyoonekana na inayoonekana katika kila pembe ya Kenya

Nyota inayong'aang'aa Afrika kuonyesha barabara sahihi

Barabara ya kimapinduzi ya kuelekea kwa uhuru

Nyota mashuhuri Afrika na hata duniani kote

Kwa wanaonyonywa na kugandamizwa

Oh pande la mwana wa Kenya, ndugu yetu mpendwa Kimaathi

Ni maneno gani tutayatumia  ewe mwana wa Waciuri

Hata tukaeleza  sifa zako tilatila kwa kikamilifu?

Ninashindwa hata kupata nahau bora

Za kuandika kuhusu Mkuu wa Jeshi la Uhuru na Mashamba

Pengine niseme tu kuwa Kimaathi alikuwa mtu

Alikuwa mtu Kimaathi, mtu kama sisi

Alikuwa na mamaye na babaye na bibiye na babuye

Alikuwa na jamaaze, damuye, kama sisi

Alikuwa na mke, mke aliempenda sana, tena sana

Kimaathi alikuwa kijana, kijana  kama sisi

Kijana alietambua jukumu lake kama mwananchi mzalendo

Mtu ambae alifahamu yu mtu kwa maneno na matendo

Kimaathi, maana ya mapenzi kwa nchi yako na watu wake

Kimaathi, mfano halisi wa ushujaa wa kimapinduzi

Ushujaa wa umma uhodari wa maslahi ya wanaogandamizwa

Kimaathi, twasira na jazanda ya kujitolea mhanga

Kwa uhuru na ukombozi wa kitaifa

Kati ya wasanii wa hila na mbinu ya vita vya kigorila

Kimaathi wa Waciuri anatajika kama msanii mkubwa

Kati ya majina yaliyokuwa yakiogopewa na wakoloni

Jina la Dedan Kimaathi lilikuwa namba wani

Kimaathi aliwafanya makaburu kujikojolea na kujiharia

Wanyonyaji wakashindwa kula manyonyaji yao kwa amani

Wangapi walowezi walifungasha na kuondoka

Kwa kuogopa Kimaathi, asakari hodari wa Mau Mau!

.....ahhhh! lakini nani asiemfahamu Kimaathi nchini!

Ni mwananchi gani mzalendo ambae hajui Mau Mau!

Ni historia gani ya Kenya hiyo ambayo haitaji Mau Mau!

Ni mashujaa gani wa Kenya unawajua kama humjui Kimaathi!

Hakika katika kuandika historia sahihi ya taifa letu

Hatutawasamehe kina Ndirangu Mau milele

Kina Ndirangu Mau- mahomugadi waliyomsaliti shujaa wetu

Kina Ndirangu Mau- kina Kenyatta na Moi wenye dola la kisaliti

Kina Ndirangu Mau- wanyonyaji wa wakulima na wafanyikazi

Kina Ndirangu Mau- vibaraka wa mabeberu

Kina Ndirangu Mau- wanaopinga ukombozi wa taifa letu

Tutawasemehe vipi kwa kuendelea kukataa kumzika Kimaathi!?

Mnamo tarehe 18  Februari, 1957

Katika Jela ya Nairobi

Dedan Kimathi wa Waciuri, shujaa mkuu wa Kenya

Alinyongwa na wakoloni wa Waingereza

Alinyongwa baada ya mateso ya kifashisti ya kina Ian Henderson

Alinyongwa huku akipambana akiwa na pingu mikononi

Shujaa wa nchi yetu alikufa akipigana

Mwili wa Kimaathi ulitupwa na wakoloni

Katika Jela ya Kamiti

Na hadi wa leo

Mazishi ya Mzalendo Kimathi

Yanangojea kufanywa, tukumbuke

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu ya kila aina

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

Mwamdawiro Mghanga, Mwenyekiti wa CPK

                                                            Jela Kuu ya Kibos    04-06-198

 

BONIFACE MWANGI, GUANTANAMO BAY, AND THE HYPOCRISY OF US SANCTIONS: STATEMENT TO...
23 May 2026 11:52

  The Communist Party Marxist Kenya notes the recent sanctions imposed by the United States government against a Tanzanian police official over the torture involving Kenyan activist Boniface Mwangi and Ugandan activist Agather Atuhaire.   As revolutionaries and defenders of democratic rights, we firmly condemn torture, arbitrary detention, repression, disappearances, and attacks against activists, workers, peasants, journalists, opposition forces, and progressive voices anywhere in Africa. The suffering of the people can never be normalised. State violence against the masses remains react [ ... ]

Read more
Fascism in the African Neocolonies Imperialist Crisis, and the Struggle for Nat...
22 May 2026 05:30

  Booker Omole, General Secretary, Communist Party Marxist Kenya
repared for the International Theoretical Conference on Fascism and Imperialism in the 21st Century in the Neocolonies
Kathmandu, Nepal
22 to 23 May 2026 Imperialism in Crisis and the Return of Fascism   The Communist Party Marxist Kenya extends militant proletarian greetings to all revolutionary organisations, communist parties, anti-imperialist formations, workers movements, youth organisations, and progressive intellectuals gathered at this important international theoretical conference in Kathmandu, Nepal.   This confe [ ... ]

Read more
STATEMENT OF THE CENTRAL COMMITTEE OF THE COMMUNIST PARTY MARXIST KENYA (CPMK) O...
19 May 2026 10:30

  The Central Committee of the Communist Party Marxist Kenya extends its highest revolutionary salute to the workers, students, boda boda riders, matatu workers, peasants, unemployed youth, and oppressed masses currently engaged in the ongoing General Strike and nationwide resistance against the unbearable conditions imposed upon the people by imperialism and its local comprador agents.   Today Kenya stands at a historic turning point.   The masses can no longer live in the old way. The ruling classes can no longer govern in the old way.   The sharp increase in fuel prices, transpo [ ... ]

Read more
THE DRIVE INTO WORLD WAR 3 AND THE WORLD ANTI IMPERIALIST FRONT
11 May 2026 07:14

  ate:  10b>th May 2026 Occasion: International Colloquium by World Anti-Imperialist Platform, Nairobi    Author: Booker Omole Position: General Secretary, Communist Party Marxist Kenya   E DRIVE INTO WORLD WAR 3 AND THE HISTORICAL EPOCH   Comrades, we are not living in ordinary times. We are living in a time of rupture, a time of transition, a time when the old order is decaying but refuses to die, and the new order is struggling to be born. The drive into a Third World War is not an accident. It is not a misunderstanding. It is not the result of individual leaders acting irr [ ... ]

Read more